Upungufu wa Nguvu za kiume


Katika siku za hivi karibuni kumekua na ongezeka kubwa la upungufu wa nguvu za kiume hasa kwa wanaume waishio maeneo ya mijini. Kwanza tunahitaji kujua kiundani nini maana ya upungufu wa nguvu za kiume chanzo chake pamoja na matibabu yake.

Upungufu wa nguvu za kiume kwa ufupi ni Mwanaume kushindwa kufanya tendo la ndoa vyema hivyo kupoteza nafasi kubwa ya upatikanaji wa mimba kwa Mwanamke.


Tatizo hili limegawanyika katika sehemu kuu 3
1.      Upungufu wa Mbegu za kiume (Low Sperm Count)
2.      Uume kushindwa kusimama Imara (Erectile Dysfunction)
3.      Kushindwa kufikia Mshindo (Prolonged ejaculation)                                                                                   

Upunguvu wa mbegu za kiume (Low Sperm Count)
Kwa kawaida wakati wa kufanya tendo la ndoa mwanaume hutoa shahawa (mchanganyiko wa mbegu za uzazi na simeni). Shahawa huwa na rangi ya maziwa iliyokoloea. Kwa mwanaume mwenye tatizo la nguvu za kiume hutoa shahawa zilizo na rangi ya maziwa za kufifia na wengine hutoa shahawa zenye rangi ya maji kabisa.

Jinsi ya kutibu aina hii ya tatizo
1.      Fanya mazoezi mara kwa mara ili kuongeza kiasi cha homoni za testosterone
2.      Kula vyakula vya kuongeza vitamin C kama matunda.
3.      Punguza au acha matumizi ya Pombe

Uume kushindwa kusimama (Erectile Dysfunction)
Mambo yanayochangia uume kushindwa kusimama ni pamoja na matumizi ya vyakula vyenye mafuta mengi, uzito uliopita kiasi, matatizo ya kisaikolojia (stress) na matumizi ya Soya na Pombe kali. Njia nzuri ya kupambana na aina hii ni kujua chanzo ni nini na kukiepuka.


Kushindwa kufikia mshindo (Prolonged Ejaculation)
Katika hali hii mwanaume hutumia muda mrefu sana kutoa shahawa na wakati mwingine shahawa hushindwa kutoka kabisa. Aina hii visababishi vyake hufanana na vile vya uume kushindwa kusimama.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Saratani ya koo la Chakula

Tiba mbadala ya vidonda vya Tumbo

Homa ya Malale (African Sleeping sickness)